Volunteering as a Chance

Volunteering has been a way for many youths in Tanzania to enter a job market, at times when there are no direct employment opportunities. By volunteering, young people get a chance to gain the first work experiences in a desired work field (add to one´s CV), prove themselves in their work (gain good reference), and connect themsselves more easily to potential job opportunities.

Young people, having graduated from their studies, can start to volunteer in a career field of their choice  and develop their career by volunteering. This is idealy enabled when parents/guardians or mentors support them with their cost of living while they are trying to get foothold in their career.

Knowing that there are young people who don´t even have a chance to get a volunteering placement or support for the whole process of volunteering while trying to get access to a job,  our Volunteering Programme in Mwanza was initiated. If you see yourself in this position or know someone who ist, feel free to contact us: info@societalnurturing.com

Review from our Volunteer Christina C.

I would like to begin by expressing my heartfelt gratitude to the donors and supporters of this remarkable volunteering programme. The organizations TAREA, JUPE HILLLS, and Msaada Foundation have had a profoundly positive impact on both the community and families here in Mwanza.
Through the TAREA programme, local fisheries have been empowered with modern fishing knowledge and techniques. They have received vital education on how overcome challenges, such as accessing startup capital and managing their fishing group more effectively. This has not only improved their livelihoods but also strengthened their resilience and independence. In addition, Msaada Foundation has made significant strides in reducing child abuse and child labor by raising awareness about the harmful effects of child labor and promoting the rights and well- being of children through community education. Overall, these organizations are creating real, meaningful changes. They are helping to reduce poverty among fishermen and protect children from exploitation and abuse. Personally, I believe this  volunteering programme is making a tremendous difference in our society,
and I am proud to be party of this mission.

The picture below shows Christina (forth person from the left) with the Group of Tuinuane Maendeleo Landing Site Mwahili in Mwanza, while volunteering at TAREA

Our Volunteers in Action

It has been a month now since we launched our volunteering programme in Mwanza. Our first volunteers, Christina, Paulo and Salum engage in contributing to the betterment of our society, while at the same time gaining practical experience in the respective fields of work. While engaging in TAREA´s renewable  energy projects (here specifically supporting fishermen/ fisherwomen) and educational work in schools (though Msaada Foundation and Jupe Hills Pre & Primary School), our programme aims to provide guidance and open up perspectives for young people for the step after their volunteering service (further studies or job market integration). We are thankful to all involved people who made this programme possible.

Volunteering Programme 2025 in Mwanza

 

With the applications from enthusiastic volunteers and the successful interviews conducted yesterday, we are excited to proceed with final preparations for the launch of our first cohort, set to begin on February 1, 2025.

This cohort will focus on school education and social work, offering participants hands-on experience while equipping them with skills to pursue meaningful opportunities post-program. As we kick off this transformative initiative, we are actively seeking sponsors to support the program financially, enabling us to engage a larger number of volunteers. This expansion would amplify the program’s impact and further our goal of integrating more youth into the job market after their volunteering experience.

For more details about our donation call and how you can contribute to this cause, please visit: Fundraising for a Volunteering Project

The second cohort is expected to start in July 2025. Application of interested young people are therefore welcome.

Fursa ya Kuinuana Kiuchumi

 

Je, unalo wazo la biashara lakini unakosa nyenzo au msaada wa kitaalamu kulitekeleza? Katika dunia inayokumbwa na changamoto ya ukosefu wa ajira, vijana wanapaswa kuwa nguzo ya mabadiliko. Kwa kutambua hili, Consultation Center for Societal Nurturing (CCSN) imeanzisha mchakato wa kusaidia vijana kama wewe kufanikisha ndoto zao za kibiashara.

Lengo letu ni kuleta suluhisho la kudumu kwa tatizo la ukosefu wa ajira, si tu kwa kuwasaidia vijana mmoja mmoja, bali pia kwa kuhakikisha kuwa jamii kwa ujumla inanufaika. Tunajua kuwa kijana mwenye fursa ya kujiajiri anaweza kugeuka kuwa chachu ya maendeleo, si kwake tu bali pia kwa wale waliomzunguka. Hivyo, tunakuwezesha katika:
• Kupata sehemu ya mtaji wa kuanzisha  biashara yako.
• Ushauri wa kitaalamu na maarifa yatakayokusaidia kusimamia biashara kwa mafanikio.
• Fursa ya kukuza mtandao wako wa kibiashara na kujifunza kupitia vijana wengine wenye mafanikio.

FURSA HII NI YAKO!
Huu ni wakati wa kuchukua hatua. Ikiwa unalo wazo la biashara, CCSN ipo hapa kukupa nguvu unayohitaji ili kulitekeleza. Tunakualika utume wazo lako la biashara pamoja na mpango kazi kwa barua pepe info@societalnurturing.com nasi tutawasiliana nawe kwa ajili ya hatua zaidi.

KWA NINI TUFANYE HAYA?
Sisi CCSN tunaamini kuwa kila kijana ana uwezo wa kuwa mshindi endapo atapewa nafasi na msaada sahihi pale anapohitaji kujikwamua kimaisha na kuiishi ndoto yake. Tunataka kuona kizazi kinachoongozwa na maarifa, ubunifu, na bidii, kikibadilisha hadithi ya ukosefu wa ajira na kuwa mfano wa mafanikio. Fursa ya kuinuana ni ya pekee, na tunaamini kuwa pamoja tunaweza kujenga jamii bora, yenye mafanikio na maendeleo endelevu.

USIKAIE HII NAFASI!
🌟 Wazo lako la leo linaweza kuwa biashara kubwa ya kesho.
🌟 Safari yako ya mafanikio inaanza na hatua moja – kutuma mpango wako kwetu.
🌟 Jiunge nasi na tufanye kazi pamoja kuleta mabadiliko makubwa.

Tutafurahi kupokea ujumbe kutoka kwako uwako.

Fundraising for a Volunteering Projekt

Hi there!

We are collecting donations for our initiative of seven non-profit organisations in Tanzanian (https://societalnurturing.com/current-projects/). With this initiative, we want to help 20 young Tanzanians into the labour market or training through voluntary service in
2025. Our programme is aimed at economically underprivileged, unemployed young people who are to be given vocational guidance in the occupational field of their choice and, with parallel career counselling and targeted networking, are to be enabled to find work or training afterwards. This opportunity does not exist in Tanzania (for Tanzanians). There is interest in this programme on the part of the young people, but it fails due to a lack of financial resources. The picture above shows a young man who was helped into the labour market thanks to our support.
With this donation, 60% of it will be used directly for the young Tanzanians as pocket money (e.g. for food, accommodation for Tanzanians from distant regions and travel costs), 40% of the donation will be used for the organisation of the voluntary service (eg. seminar costs, educational support and material costs). A fair application and selection process is used to choose the beneficiaries. Donors are welcome to receive regular updates on the progress of the project or to make an on-site visit. We will be happy to answer any queries.

We shared this link on gofundme-page as well (though in German language):
https://gofund.me/4fd2e569

Thank you in advance for your willingness and support and sharing this information with other potential supporters

Forum

We are currently developing a forum with topics which fits the needs of young Tanzanian. If you are interested in being part of the forum, feel free to leave a message via info@societalnurturing.com

As soon as our forum is establish you will be invited to join.

 

Fursa ya Mikopo bila Riba kwa ajili ya Biashara

Je, wajua kuwa unaweza kupata bila riba kwa ajili ya kuendesha shughuli zako za kiuchumi? Basi endelea kusoma makala hii kupata taarifa zaidi.

Hivi karibuni, Halmashauri zote za Tanzania zimeweka mkazo katika kutoa mikopo isiyokuwa na riba kwa makundi maalum kama vile wanawake, vijana (miaka 18 -35), na watu wenye ulemavu. Hii imefanyika kwa kutoa asilimia kumi ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kila kundi, huku wanawake wakipewa asilimia nne, vijana asilimia nne, na watu wenye ulemavu asilimia mbili. Hatua hii inalenga kuchochea ujasiriamali na maendeleo ya kiuchumi katika makundi haya, huku ikiondoa kabisa gharama ya riba.

ZIFUATAZO NDIO VIGEZO VYA KUSTAHIKI KUPATA MKOPO:

Ili kustawisha kutolewa kwa mikopo isiokuwa na riba, kuna vigezo muhimu ambavyo kundi linalokusudiwa kupata mkopo linapaswa kukidhi. Hii ni hatua muhimu kuhakikisha kwamba mikopo inawafikia wale wanaoihitaji na inachangia katika maendeleo ya ujasiriamali na shughuli za kiuchumi. Hapa chini ni orodha ya vigezo hivyo: Kumbuka, vigezo hivi ni kwa Halmashauri zote za Tanzania.

Ujasiriamali na Nia ya Kuanzisha Shughuli za Kiuchumi: Kundi linapaswa kuonyesha jitihada za kujishughulisha katika ujasiriamali au kuwa na nia ya kuanzisha shughuli za kiuchumi.

Ukubwa wa Kundi: Kwa vikundi vya wanawake au vijana, linapaswa kuwa na wanachama kumi au zaidi. Kwa upande wa watu wenye ulemavu, vikundi visiwe chini ya watano wala kuzidi kumi. Hii inalenga kuwahusisha wengi iwezekanavyo katika fursa hii.

Akaunti ya Benki: Kundi linapaswa kuwa na akaunti ya benki kwa jina la kikundi. Hii ni hatua muhimu katika usimamizi wa fedha na kudumisha uwazi katika matumizi ya mikopo.

Ukosefu wa Ajira Rasmi: Wanachama wa kikundi wasiwe na ajira rasmi. Hii inasisitiza lengo la mikopo isiokuwa na riba kusaidia wale ambao wanaweza kukosa ufikiaji wa mikopo kwa njia za kawaida.

Raia wa Tanzania na Umri: Wanachama wanapaswa kuwa raia wa Tanzania wenye umri wa miaka kumi na nane au zaidi. Hii inahakikisha kwamba mikopo inawalenga wale ambao wana haki ya kisheria kuingia mikataba ya kifedha.

MAOMBI YA MKOPO:

kikundi kinachotamani kupata mkopo kitapaswa kuanza safari yake kwa kujaza fomu maalum ya maombi. Fomu hii itatolewa na Halmashauri husika. Baada ya kujaza kwa makini fomu ya maombi, hatua muhimu inayofuata ni kuambatisha nyaraka zinazounga mkono ombi. Hii ni hatua ya muhimu katika kuhakikisha ufanisi wa mchakato wa maombi. Kwa mfano, kikundi kinahitajika kuambatanisha nakala za katiba yake, cheti cha usajili wa kikundi, na, ikiwa kinafanya biashara, leseni ya biashara.

Vilevile, ni muhimu kutoa nakala halisi za taarifa za akaunti kutoka benki ambayo kikundi kina akaunti. Hii itathibitisha utaratibu wa kifedha wa kikundi. Barua za utambulisho kutoka kwa Mtendaji wa Kijiji au Mtaa pamoja na Mtendaji wa Kata zinahitajika kama uthibitisho wa uwepo wa kikundi katika eneo husika. Pia, kutoa wazo la biashara kunahitajika kueleza kwa kina shughuli za biashara ambazo kikundi kinataka kutekeleza. Halmashauri itakuwa mshirika wa karibu katika mchakato huu. Baada ya kupokea maombi, Halmashauri ina jukumu la kutoa taarifa ya kupokea ombi hilo kwa kikundi husika ndani ya siku tatu. Hii ni hatua muhimu inayowawezesha waombaji kujua kuwa hatua yao ya kwanza imefanikiwa.

Muda wa Kushughulikia Maombi ya Mikopo: Halmashauri imechukua jukumu la kuhakikisha mchakato wa maombi ya mikopo unakamilika kwa ufanisi na haraka. Kipindi cha kushughulikia maombi hakitaenda zaidi ya miezi mitatu tangu siku ya kupokelewa kwa maombi hayo. Kwa kuongezea, jukumu la Halmashauri halimalizi tu na kushughulikia maombi. Wanachukua hatua ya ziada kuhakikisha fedha zinaelekezwa mahali sahihi. Mara tu vikundi vinapokidhi vigezo na kusaini mkataba wa makubaliano, Halmashauri ina jukumu la kupeleka fedha hizo kwa haraka katika akaunti za vikundi husika.

Marejesho: Mkopo uliotolewa kwa kikundi utatakiwa kuanza kurejeshwa baada ya muda wa miezi mitatu tangu siku ya kupata mkopo. Hii inamaanisha kuwa vikundi vitapewa muda wa “grace period” kama wanavyosema wamombo wa miezi mitatu bila kulazimika kuanza marejesho. Baada ya kipindi hiki, vikundi vitahitajika kuanza mchakato wa kurejesha mikopo yao kwa mujibu wa makubaliano. Muda huu wa miezi mitatu unalenga kuwapa wakopaji muda wa kuanzisha au kuimarisha shughuli zao za biashara kabla ya kuanza kurejesha mkopo. Hii ni hatua inayosaidia kuhakikisha kwamba vikundi vinapata fursa ya kujipanga kifedha na kuepuka shinikizo la malipo mapema.

HITIMISHO

Kupitia mpango huu wa mikopo bila riba, wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu wana fursa mpya zenye manufaa makubwa. Faida za mpango huu ni dhahiri, kwani unawawezesha kujenga biashara zako bila mzigo wa riba, huku ukipata mtaji wa kuanzia. Hii sio tu inakupa nguvu za kifedha, bali pia inaleta ufanisi katika jamii kwa kuchochea ujasiriamali na maendeleo ya kiuchumi. Fursa hii inawawezesha kuchangia katika ukuaji wa jamii  na kuwa nguvu inayosukuma mbele ustawi wa pamoja. Tembelea Halmashauri yako kwa taarifa na ushauri zaidi.

Iwapo utahitaji msaada katika kupata mkopo huu, hususan katika kuandika katiba au mpango wa biashara, karibu uwasiliane nasi. Iwapo tayari umeshapata mkopo huu, tutafurahi kusikia kuhusu uzoefu wako. Kama unahitaji kuboresha biashara yako ili kuimarisha kipato na kujihakikishia kiwango cha marejesho ya mkopo, tutafurahi kushiriki kukusogeza hatua nyingine ya mafanikio

Mradi wa Biashara – Matunda ya Kukausha

CCSN imeanzisha mradi mdogo wa kukausha matunda na kuyauza kama kitafunwa cha asili (bila kuongeza sukari au kemikali) na hivyo kutengeneza ajira kwa vijana na kuepusha uharibiribifu wa matunda ya msimu, hasa maembe na mananasi. Baada ya kufanikisha zoezi la kukausha na kupata miitikio chanya kutoka kwa watu, tuko sasa katika utaratibu na maandalizi ya usajili wa biashara hiyo kupitia SIDO na TBS.

Kitafunwa hiki kimepata mwitikio mzuri kwa watoto na hata kwa watu wazima, kama kiburudisho, kionjo, kipoza njaa au kama zawadi kwa mtu. Pembeni na vitanfunwa tunavyovifahamu, kama vile karanga, korosho, bisi au bisukuti, sasa tumeongeza kingine kinachotokana na matunda yetu ya asili. Kama una shauku ya kujaribu bidhaa yetu, kushiriki katika biashara yetu au hata kutupatia maoni yoyote, karibu uwasiliane nasi.