Fursa ya Mikopo bila Riba kwa ajili ya Biashara

Je, wajua kuwa unaweza kupata bila riba kwa ajili ya kuendesha shughuli zako za kiuchumi? Basi endelea kusoma makala hii kupata taarifa zaidi.

Hivi karibuni, Halmashauri zote za Tanzania zimeweka mkazo katika kutoa mikopo isiyokuwa na riba kwa makundi maalum kama vile wanawake, vijana (miaka 18 -35), na watu wenye ulemavu. Hii imefanyika kwa kutoa asilimia kumi ya mapato ya ndani ya Halmashauri kwa kila kundi, huku wanawake wakipewa asilimia nne, vijana asilimia nne, na watu wenye ulemavu asilimia mbili. Hatua hii inalenga kuchochea ujasiriamali na maendeleo ya kiuchumi katika makundi haya, huku ikiondoa kabisa gharama ya riba.

ZIFUATAZO NDIO VIGEZO VYA KUSTAHIKI KUPATA MKOPO:

Ili kustawisha kutolewa kwa mikopo isiokuwa na riba, kuna vigezo muhimu ambavyo kundi linalokusudiwa kupata mkopo linapaswa kukidhi. Hii ni hatua muhimu kuhakikisha kwamba mikopo inawafikia wale wanaoihitaji na inachangia katika maendeleo ya ujasiriamali na shughuli za kiuchumi. Hapa chini ni orodha ya vigezo hivyo: Kumbuka, vigezo hivi ni kwa Halmashauri zote za Tanzania.

Ujasiriamali na Nia ya Kuanzisha Shughuli za Kiuchumi: Kundi linapaswa kuonyesha jitihada za kujishughulisha katika ujasiriamali au kuwa na nia ya kuanzisha shughuli za kiuchumi.

Ukubwa wa Kundi: Kwa vikundi vya wanawake au vijana, linapaswa kuwa na wanachama kumi au zaidi. Kwa upande wa watu wenye ulemavu, vikundi visiwe chini ya watano wala kuzidi kumi. Hii inalenga kuwahusisha wengi iwezekanavyo katika fursa hii.

Akaunti ya Benki: Kundi linapaswa kuwa na akaunti ya benki kwa jina la kikundi. Hii ni hatua muhimu katika usimamizi wa fedha na kudumisha uwazi katika matumizi ya mikopo.

Ukosefu wa Ajira Rasmi: Wanachama wa kikundi wasiwe na ajira rasmi. Hii inasisitiza lengo la mikopo isiokuwa na riba kusaidia wale ambao wanaweza kukosa ufikiaji wa mikopo kwa njia za kawaida.

Raia wa Tanzania na Umri: Wanachama wanapaswa kuwa raia wa Tanzania wenye umri wa miaka kumi na nane au zaidi. Hii inahakikisha kwamba mikopo inawalenga wale ambao wana haki ya kisheria kuingia mikataba ya kifedha.

MAOMBI YA MKOPO:

kikundi kinachotamani kupata mkopo kitapaswa kuanza safari yake kwa kujaza fomu maalum ya maombi. Fomu hii itatolewa na Halmashauri husika. Baada ya kujaza kwa makini fomu ya maombi, hatua muhimu inayofuata ni kuambatisha nyaraka zinazounga mkono ombi. Hii ni hatua ya muhimu katika kuhakikisha ufanisi wa mchakato wa maombi. Kwa mfano, kikundi kinahitajika kuambatanisha nakala za katiba yake, cheti cha usajili wa kikundi, na, ikiwa kinafanya biashara, leseni ya biashara.

Vilevile, ni muhimu kutoa nakala halisi za taarifa za akaunti kutoka benki ambayo kikundi kina akaunti. Hii itathibitisha utaratibu wa kifedha wa kikundi. Barua za utambulisho kutoka kwa Mtendaji wa Kijiji au Mtaa pamoja na Mtendaji wa Kata zinahitajika kama uthibitisho wa uwepo wa kikundi katika eneo husika. Pia, kutoa wazo la biashara kunahitajika kueleza kwa kina shughuli za biashara ambazo kikundi kinataka kutekeleza. Halmashauri itakuwa mshirika wa karibu katika mchakato huu. Baada ya kupokea maombi, Halmashauri ina jukumu la kutoa taarifa ya kupokea ombi hilo kwa kikundi husika ndani ya siku tatu. Hii ni hatua muhimu inayowawezesha waombaji kujua kuwa hatua yao ya kwanza imefanikiwa.

Muda wa Kushughulikia Maombi ya Mikopo: Halmashauri imechukua jukumu la kuhakikisha mchakato wa maombi ya mikopo unakamilika kwa ufanisi na haraka. Kipindi cha kushughulikia maombi hakitaenda zaidi ya miezi mitatu tangu siku ya kupokelewa kwa maombi hayo. Kwa kuongezea, jukumu la Halmashauri halimalizi tu na kushughulikia maombi. Wanachukua hatua ya ziada kuhakikisha fedha zinaelekezwa mahali sahihi. Mara tu vikundi vinapokidhi vigezo na kusaini mkataba wa makubaliano, Halmashauri ina jukumu la kupeleka fedha hizo kwa haraka katika akaunti za vikundi husika.

Marejesho: Mkopo uliotolewa kwa kikundi utatakiwa kuanza kurejeshwa baada ya muda wa miezi mitatu tangu siku ya kupata mkopo. Hii inamaanisha kuwa vikundi vitapewa muda wa “grace period” kama wanavyosema wamombo wa miezi mitatu bila kulazimika kuanza marejesho. Baada ya kipindi hiki, vikundi vitahitajika kuanza mchakato wa kurejesha mikopo yao kwa mujibu wa makubaliano. Muda huu wa miezi mitatu unalenga kuwapa wakopaji muda wa kuanzisha au kuimarisha shughuli zao za biashara kabla ya kuanza kurejesha mkopo. Hii ni hatua inayosaidia kuhakikisha kwamba vikundi vinapata fursa ya kujipanga kifedha na kuepuka shinikizo la malipo mapema.

HITIMISHO

Kupitia mpango huu wa mikopo bila riba, wanawake, vijana, na watu wenye ulemavu wana fursa mpya zenye manufaa makubwa. Faida za mpango huu ni dhahiri, kwani unawawezesha kujenga biashara zako bila mzigo wa riba, huku ukipata mtaji wa kuanzia. Hii sio tu inakupa nguvu za kifedha, bali pia inaleta ufanisi katika jamii kwa kuchochea ujasiriamali na maendeleo ya kiuchumi. Fursa hii inawawezesha kuchangia katika ukuaji wa jamii  na kuwa nguvu inayosukuma mbele ustawi wa pamoja. Tembelea Halmashauri yako kwa taarifa na ushauri zaidi.

Iwapo utahitaji msaada katika kupata mkopo huu, hususan katika kuandika katiba au mpango wa biashara, karibu uwasiliane nasi. Iwapo tayari umeshapata mkopo huu, tutafurahi kusikia kuhusu uzoefu wako. Kama unahitaji kuboresha biashara yako ili kuimarisha kipato na kujihakikishia kiwango cha marejesho ya mkopo, tutafurahi kushiriki kukusogeza hatua nyingine ya mafanikio

Mradi wa Biashara – Matunda ya Kukausha

CCSN imeanzisha mradi mdogo wa kukausha matunda na kuyauza kama kitafunwa cha asili (bila kuongeza sukari au kemikali) na hivyo kutengeneza ajira kwa vijana na kuepusha uharibiribifu wa matunda ya msimu, hasa maembe na mananasi. Baada ya kufanikisha zoezi la kukausha na kupata miitikio chanya kutoka kwa watu, tuko sasa katika utaratibu na maandalizi ya usajili wa biashara hiyo kupitia SIDO na TBS.

Kitafunwa hiki kimepata mwitikio mzuri kwa watoto na hata kwa watu wazima, kama kiburudisho, kionjo, kipoza njaa au kama zawadi kwa mtu. Pembeni na vitanfunwa tunavyovifahamu, kama vile karanga, korosho, bisi au bisukuti, sasa tumeongeza kingine kinachotokana na matunda yetu ya asili. Kama una shauku ya kujaribu bidhaa yetu, kushiriki katika biashara yetu au hata kutupatia maoni yoyote, karibu uwasiliane nasi.

Jinsi ya Kukuza na Kutanua Biashara yako Kidijitali

“Nenda na wakati”, msemo unaopata uzito zaidi katika ulimwengu wa biashara ya leo. Kwa wafanyabiashara wa Tanzania, kuchukua hatua zinazokwenda sambamba na mabadiliko ya kiteknolojia ni muhimu sana. Kupitia njia za ubunifu, tunaweza kujenga mustakabali wa biashara zetu na kuleta mabadiliko chanya katika utendaji wetu. Hii ni fursa ya kipekee ya kuboresha mchakato wa biashara, kuongeza wigo wa wateja, na kuimarisha utendaji wa jumla. Katika makala hii, tutajadili jinsi ya kutumia teknolojia kwa njia bora ili kuleta mabadiliko chanya kwenye biashara yako.

Masoko ya Kidijitali (Digital Marketing) ni mkakati wa kutafuta masoko na kujitangaza kupitia njia za kidigitali ili kufikia, kushirikiana, na kuwavuta wateja mtandaoni. Hii inajumuisha matumizi ya anuwai ya majukwaa na zana za mtandao kama vile tovuti, mitandao ya kijamii, barua pepe, blogu, na matangazo ya mtandaoni. Lengo la soko la kidijitali ni kuongeza uwepo wa biashara, kuimarisha uhusiano na wateja, na hatimaye, kuongeza mauzo na mapato.

Mambo matatu muhimu kuzingatia ili kukuza biashara yako kidijitali ni:

  1. Tumia Mtandao wa Kijamii: Kuanzisha uwepo wa kijamii mtandaoni kunaweza kuwa hatua kubwa kwa wafanyabiashara wadogo na wakubwa pia. Kutumia majukwaa kama Facebook, Instagram, na Twitter kutoa taarifa kuhusu bidhaa au huduma zako kunaweza kuvutia wateja wapya na kuwawezesha wateja wako wa sasa kushirikiana nawe moja kwa moja. Na haikugharimu. Leo, inapokuja kwenye kutafuta msaada au habari, simu za mkononi zinaendelea kuwa chombo cha kwanza cha watu. Kupitia kuperuzi mtandaoni, majibu ya maswali na suluhisho kwa matatizo yanapatikana haraka na kwa urahisi. Lakini je, wewe kama mfanyabiashara ukiwa nje ya mtandao, ni kwa jinsi gani watu watakujua? Je, ni kwa namna gani watagundua kuwa una biashara sehemu fulani? Nenda na wakati, ingia kwenye ulimwengu wa dijitali.

Fikiria mfanyabiashara wa samani (Furniture), Bwana Ahmed, ambaye ana biashara yake inayoitwa “Elegance Furniture.” Ahmed amechukua hatua kubwa katika kukuza biashara yake kwa kutumia mtandao wa kijamii. Kupitia majukwaa kama Facebook, Instagram, na Twitter, Elegance Furniture inaonyesha kwa kina na ubunifu samani zake za kipekee. Ni muhimu kufahamu kuwa kufungua akaunti kwenye mitandao ya kijamii ni rahisi na haichukui muda mrefu. Bwana Ahmed anaweza kuanzisha akaunti hizo kwa kujaza habari muhimu kuhusu biashara yake, kuchagua picha nzuri za bidhaa zake, na kuanza kushirikisha na wateja. Kupitia ukurasa wake katika mtandao wa jamii, anweza kuionnesha mitindo mbalimbali, rangi, na ubora wa kazi zake, na kutumia matangazo ya moja kwa moja kwenye majukwaa haya hata kutoa ofa maalum kwa wafuasi wake. Hatua hizi za kuanzisha akaunti ni rahisi na hazihitaji ujuzi wa kitaalamu wa kiteknolojia. Kwa hiyo, Bwana Ahmed anaweza kufanya hivyo kwa haraka na kwa gharama nafuu.

Leo, wateja wapendeleao samani wanaweza kuperuzi ukurasa wa Instagram wa Elegance Furniture na kushiriki maoni yao moja kwa moja. Hii inawapa wateja nafasi ya kushirikiana na mfanyabiashara, kuuliza maswali, na hata kupata ushauri wa kitaalam kuhusu chaguo la samani bora kwa nyumba zao.

Kwa kufanya hivyo, Elegance Furniture inakuwa sio tu mfanyabiashara wa samani bali pia jukwaa la mawasiliano na burudani kwa wateja wake. Hii inaongeza uhusiano na wateja, inavutia wapenzi wa samani, na inawawezesha wateja wa sasa na wapya kugundua na kununua bidhaa zao kwa urahisi. Kwa kubadilika na kuingia kwenye ulimwengu wa dijitali, Elegance Furniture inaonyesha njia bora za kuvutia wateja na kukuza biashara ya samani.

  1. Anzisha Duka la Mtandaoni: Kupitia majukwaa ya e-commerce, kama vile Shopify, Jiji, Zoom Tanzania, n.k. wafanyabiashara wanaweza kuongeza uwezo wa kufikia wateja wapya na wa mbali. Kuanzisha duka la mtandaoni kunaweza kuongeza mapato na kuwawezesha wateja kununua bidhaa au huduma zako popote walipo.

Hapa tutatumia mfano nadharia wa mfanyabiashara wa bidhaa za asili, “Asilia Delights”. Ni hatua zipi anaweza kuzifuata kupitia maduka ya mitandanoni na kukuza biashara yake nje ya mipaka yake ya kila siku:

Mtu kama Anna, anayependa bidhaa za asili na anayetafuta njia rahisi ya kujipatia taarifa zaidi na kununua bidhaa hizo bila kuhitaji kwenda dukani, anaweza kuvutiwa na mfanyabiashara wa bidhaa za asili ambaye amejikita katika kuuza bidhaa zake kwa njia ya mtandaoni. Mfano mzuri ni Biashara ya “Asilia Delights,” inayojikita katika kutoa bidhaa za asili kama vile mafuta ya ngozi, sabuni za asili, na bidhaa za nywele.

Asilia Delights inachagua jukwaa la e-commerce kama Shopify au Zoom Tanzania kuanzisha duka lake la mtandaoni. Tovuti yao inavutia na ina muundo rahisi na maelezo mazuri ya bidhaa. Anna anapofika kwenye tovuti, anapata habari kamili kuhusu jinsi bidhaa hizo za asili zinavyomfaa, na hata ana fursa ya kusoma blogi inayoelezea faida za kutumia bidhaa hizo za asili katika maisha ya kila siku.

Kwa kufurahishwa na maelezo na ubora wa bidhaa kwenye tovuti, Anna anachagua bidhaa anazotaka na anaweza kulipia kwa urahisi kupitia huduma za malipo mkondoni kama M-Pesa, hivyo kupokea bidhaa zake kwa haraka kupitia usafiri utakaokuwa umeandaliwa. Asilia Delights pia inamhamasisha Anna kushiriki ununuzi wake kwenye mitandao ya kijamii, na wanatoa ofa maalum kama vile punguzo kwa wanunuzi wa kwanza au zawadi kwa ununuzi wa kiasi fulani.

Biashara hii pia inaweza kutumia ushawishi wa jamii (influencer marketing) kwa kushirikiana na wataalamu wa urembo wa asili wanaopenda bidhaa zao. Wapo Mwanablogu maarufu katika kila fani wanaotoa mapitio katika bidhaa husika na hivyo kuongeza inaongeza uaminifu na kuvutia wateja wapya kwa bidhaa hizo. Kuwasiliana na wanablog hao, huweza kufungua njia ya ushirikiano katika biashara.

Duka la mtandaoni pia hutoa njia za mawasiliano kama vile barua pepe na chat moja kwa moja kwa wateja, ikidhihirisha jitihada za kutoa huduma bora kwa wateja. Kwa kufanya hivyo, mfanyabiashara anafanya duka lake liwe na mvuto, likiendelea kueneza bidhaa zake hata nje ya mipaka ya biashara yake.

Wakati wa kujenga bajeti ya biashara ya mtandaoni, ni muhimu kuelewa kwamba kuanzisha duka la mtandaoni kunahusisha gharama ambazo wewe mfanyabiashara lazima uzizingatie. Gharama hizi ni pamoja na ada za usajili wa jukwaa la e-commerce, gharama za uendeshaji wa tovuti au duka la mtandaoni, na malipo ya huduma za malipo mkondoni. Aidha, mfanyabiashara unaweza kukutana na gharama za masoko mtandaoni, ambazo zinaweza kujumuisha matangazo na kukuza bidhaa ili kuvutia wateja pamoja na gharama za kuwalipa influencers kama sehemu ya mkakati wa masoko.

  1. Huduma za Malipo Mkondoni (online payments): Kutumia njia za malipo mkondoni kunaweza kuharakisha mchakato wa mauzo na kutoa urahisi kwa wateja. Huduma kama vile M-Pesa, Tigo Pesa, na malipo ya kadi zinaweza kutumika kuwezesha malipo salama na haraka.

Fikiria biashara ya “Mzuri Salon Supplies,” inayomilikiwa na Mary, ambayo inajihusisha na usambazaji wa vifaa vya urembo na nywele kwa saluni na wauzaji wa bidhaa za urembo nchini Tanzania. Mary amechagua kuanzisha uwepo wa mtandaoni kupitia duka lake la mtandaoni ili kufikia wateja kote nchini.

Mteja wake, Ana, aliye mbali na eneo la biashara ya Mary, anaweza kutembelea tovuti ya Mzuri Salon Supplies na kuchagua bidhaa anazotaka. Kwa kutumia huduma za malipo mkondoni kama M-Pesa, Ana anaweza kufanya malipo kwa urahisi bila haja ya kufika moja kwa moja kwenye duka la Mary. Hii inaharakisha mchakato wa ununuzi na kumwezesha Ana kununua bidhaa hizo hata akiwa mbali.

Huduma za malipo mkondoni zinawapa wafanyabiashara kama Mary fursa ya kutoa njia salama, rahisi, na haraka za malipo kwa wateja wao. Hii inaongeza ufanisi wa mchakato wa mauzo na kutoa urahisi kwa wateja ambao wanaweza kuwa mbali na eneo la biashara. Kwa njia hii, Top of FormKupata wateja kama Ana, ambao wapo mbali na biashara, inaleta faida kadhaa kwako mfanyabiashara. Kwanza, inaongeza wigo wa soko na kuwezesha kufikia wateja kote nchini. Pili, huduma za malipo mkondoni hufanya mchakato wa ununuzi kuwa rahisi na haraka kwa wateja, hivyo kuongeza ufanisi na kutoa uzoefu bora wa ununuzi. Tatu, inarahisisha usafirishaji wa bidhaa kwa kufanya mawasiliano kati ya biashara na wateja kuwa ya moja kwa moja. Hii yote inachangia kuimarisha uhusiano na wateja, kuongeza mapato, na kujenga sifa bora kwenye soko la mtandaoni.

Hitimisho

Kukuza biashara kwa njia ya kidigitali inahitaji mipango imara na ubunifu wa kibiashara ili kujitofautisha katika ushindani mkubwa wa soko. Hatua muhimu ni pamoja na kuandaa mipango ya mkakati wa kidigitali, kuboresha tovuti na huduma za mtandaoni, kutumia masoko ya mtandao wa kijamii kwa ufanisi, kufahamu washindani, kutoa huduma bora kwa wateja mtandaoni, kutumia teknolojia za kisasa, na kutoa huduma za kipekee. Kwa kufanya hivyo, biashara inaweza kupenya mipaka ya kijiografia, kufikia wateja wapya, na kustawi katika mazingira ya biashara ya kidigitali.

Anza sasa. Dunia inakua kwa kasi, na fursa za kukuza biashara yako zinakusubiri. Kwa kutumia teknolojia, unaweza kuongeza wigo wa wateja, kuboresha ufanisi, na kuvunja vizuizi vya kijiografia. Hivyo, nenda na wakati, na angalia jinsi teknolojia inavyoweza kuongeza thamani kwa biashara yako. Hakuna wakati bora wa kuchukua hatua kuelekea mafanikio ya biashara yako ya ndoto.

 

 

Timiza Ndoto Zako kupitia Biashara

Kuanzisha na kuendesha biashara inayopendwa na yenye mafanikio ni shauku ya vijana wengi. Changamoto katika kuanzisha, kuendesha na hata kuimarisha biashara tunazifahamu. Swala la kuendesha biashara limekuwa schangamoto kwa wengi kiasi kwamba wengi wanaofanikiwa kuendesha biashara, wameshindwa kujikimu kimaisha kutokana na mapato duni ya biashara zao. Takwimu zilizotolewa na Shamchiyeva, Kizu na Kahyarara kupitia shirikia la kazi duniani (ILO) linaonesha wastani wa mapato ya vijana wa kiume ni Tsh. 117,000/= kwa mwezi na kwa vijana wa kike ni 90,000/=. Japokuwa hizi takwimu zina miaka karibia kumi sasa, hata kama wastani umepanda kwa sasa ukilinganisha ni kipindi cha utafiti, haitoshi kujikimu kimaisha. Ukipiga hesabu ya pesa mtu anayohitaji kijikumu kimaisha kwa (ikihusisha chakula, kodi, usafiri, mawasiliano, afya na huduma tofauti tofauti – hata kama zinatofautianana maeneo na maeneo) lazima kiwango kisipungue laki tatu.

Wakati vijana wengi wakitafuta uhuru wa kiuchumi, kujitegemea na kuongeza kipato kupitia biashara, asilimia yao kubwa huingia kwenye biashara kwa sababu ya kukosa ajira. Changamoto hii huambatana na vijana wengi kutopangilia biashara yao vizuri – kuanzia kulenga wateja, mipango ya biashara ya muda mfupi na mrefu, na utekelezaji wa biashara hizo, kama Isai Mathias anavyoweka wazi katika waraka wake kuhusu sababu ya biashara  nyingi kufeli. Changamoto zinigine kama ukosefu wa mtaji, elimu, na uzoefu, mikopo yenye riba kubwa, upanuaji wa biashara kwa pupa, matumizi ya pesa ya biashara kwa ajili ya mahitaji binafsi, eneo baya ya biashara, na uendeshaji duni tunayafahamu.

Wakati huo huo tunafahamu kuwa uanzishaji und uendeshaji wa bia biashara – hasa kwa Tanzania ambapo mazingira huruhusu na sheria hazibani, ni fursa kubwa ya kufanya mambo na kutimiza ndoto binafsi.

Tunatambua kuwa sio kila mtu anaweza kuendesha biashara. Sio kila mtu atakuza biashara. Unaweza kutathmini uzuji/uwezo ulionao, sifa binafsi (k.v. motisha, hali ya uchumi), athari zinazoweza kujitokeza, na hali halisi, na kuchagua biashara inayokidhi mahitaji ya watu unaowalenga. Sifa hizi unaweza kujipatia. Kama unahitaji mwongozo zaidi katika kuanzisha biashara yenye mafanikio na inayoendana na mazingira uliyonayo, usisite kuwasiliana nasi. Kama unahitaji kuhudhuria mafunzo na kujijengea sifa kwa ajili ya biashara bora, usisite pia kuwasiliana nasi.

Fursa za Kujiajiri Tanzania

Lengo la makala hii ni kukuwezesha kuanza biashara mara moja na kuifanikisha,  iwapo utaamua. Hivyo karibu uisome makala hii mpaka mwisho.

Kama inavyofahamika, swala la mtaji, ujuzi, usimamizi mzuri na kutambua/kutengeneza fursa ni misingi muhimu katika uendeshaji wa biashara. Mara nyingi biashara zinakwama katika msingi hii.  Hebu tafakari jambo hili:

Fundi anapokuwa anashidwa kuhakikisha kazi ya mteja imefanyika wa uzuri na kwa wakati, huathiri kipato chake na ukuaji wa biashara yake. Mategemeo ya faida ya haraka na ukosefu wa nidhamu katika matumizi ya pesa ya biashara, hupelekea kutumia sehemu ya pesa ya biashara katika mahitaji binafsi (k.v. matibabu, chakula, ada ya shule) au hata kupunguza kuwekeza muda wa kutosha katika biashara. Katika mazingira haya, biashara hubaki kuwa duni.

Huenda umeshafirikia ni biashara gani ungependa kuianzisha na vigezo unavyohitaji kuvitimiza ili kufanikisha biashara hiyo. Umetathimini soko na kuona kuna fursa au uhitaji mkubwa ya bidhaa au huduma unayotaka kuitoa na pesa unayolenga kuipata. Kanuni iongozayo ni uhitaji wa bidhaa au huduma yako. Kama hakuna uhitaji mkubwa, hiyo biashara haiwezi ikajiendesha na kukidhi mahitaji yako. Panapokuwa na uhitaji mkubwa, una uhakika wa wateja. Wakati mwingine inakuhitaji kujihakishia wateja wa awali na kuwa na mzunguko mdogo wa pesa ili kuimarisha biashara yako, kabla haujabobea katika hiyo biashara na kuwekeza muda na pesa zaidi, au hata kusitisha shughuli zako zingine.

Biashara nyingi zinahitaji mtaji, ila sio zote. Kwa mfano biashara zinazotumia ujuzi wako na sisizohitaji ofisi kama, kufundisha au kusuka, hazihitaji mtaji. Hivyo, tafakari kuhusu gharama unazoweza kuziepuka katika kuanzisha biarashara yako.

Ujuzi wa kazi katika bishara ni muhimu. Mwalimu anayefundisha shule haitaji kufahamu utaratibu wa makato ya serikali, vibali na gharama za uendeshaji, namna ya kupata na kuwafikia wateja na kutengeneza mfumo mzuri wa uendeshaji wa kituo au kutengeneza mikataba. Mwalimu anayeendesha kituo cha tuisheni kwa upande mwingine hupaswa kufahamu haya. Hivyo unapoanzisha biashara yako, tafakari kuhusu mambo unayopaswa kuyajua kabla ya kuanza.

Je, katika biashara unayokusudia na una ujuzi wa kutosha? Unahitaji ujuzi kuhusu namna ya kujipatia wateja na kukuza biashara yako kupitia mtandao? Ni kweli, si lazima ujue kila kitu ili uanze biashara ila unapaswa kutambua mipaka yako katika kufikia malengo uliyoweka. Kupitia mafunzo, marafiki, washauri au hata wafanyabiashara wenza, unaweza kuziba hilo pengo.

Ili kufikia malengo, usimamizi unapaswa kuwa mzuri. Usimamizi huusisha mipango ya muda mfupi na mrefu. Pamoja na namna ya kufikia malengo hayo, juhudi na usimamizi katika kufikia malengo hayo, watu/wafanyakazi watakaosaidia kufika malengo hayo, uongozi na ukaguzi wa kazi, pamoja na maamuzi thabiti pale ambapo malengo husika hayajafikiwa, ni mambo ya msingi ya kuzingatia.

Pale ambapo unakuwa hauko makini katika kutimiza malengo ya biashara, kutoweka mbinu za kutimiza kazi hata wakati wa dharura, lazima kutambua athari yake katika biashara na kipato chako. Unapochagua ndugu au marafiki kama wafanyakazi bila kuweka kipaumbele katika uwezo na elimu yao, bila kuzingatia mgongano wa masilahi katika kukamilisha malengo yako ya biashara na kupata ujuzi unaohitaji, ni rahisi kuwa na biashara isiyoendelea. Sio lazima kumuajiri mtu na kufanya kazi naye, ili uweze kumsaidia. Biashara nyingi za kusaidiana zinabaki katika hali ya chini, hazikidhi gharama ya uendeshaji na mahitaji. Wengi wanaishia kuomba omba na kukopa, lisha ya kuwa wana biashara. Kuna watu wanaokubali tenda ili wapate pesa ya kufanya kazi ya mteja mwingine na kupata hela ya kula. Mazingira haya yamefanya biashara zetu nyingi kuwa katika hali duni.

La mwasho – biashara nyingi hushindwa kufanyika kwa sababu ya kusingizia vikwazo vya mtaji, ujuzi au mifumo duni (sheria n.k.). Visingizio hivi havisaidii pale tunapotafuta suluhisho hata kwa kuanza taratibu.

Mfano: kama ninahitaji kufungua stationery na sina mtaji wa milioni 3 au siwezi kupata kwa ndugu/marafiki, naweza kuona pa kuanzia huku nikiweka mpango thabiti namna ya kufikia lengo hilo, hata kama likichukua muda zaidi. Naweza nikaangalia pa kuanzia kulingana na mahitaji ya wateja hali nikijua sitaweza kuitegemea hiyo biashara riziki ya kila siku. Mahitaji ya wateja yaweza kuwa madaftari, kalamu, nitanunua vitu hivyo  na kuuzia wateja huku huku nikiendelea kuzingatia mahitaji zaidi na  kukuza mtaji wangu. Naweza pia kutumia Kompyuta ya mtu kuchapa kazi za wateja. Njia hii ndefu ni uwekezaji, haupaswi kutegemewa kama riziki, lakini husadia kufikia malengo

Mfano wa pili: Kama ninahitaji pikipiki kama kitega uchumi ila sina hela, naweza

  1. Kuunganisha nguvu na mtu/watu (njia ya haraka)
  2. Kukusanya pesa taratibu kwa ajili ya pikipiki nitakayoimudu baadaye
  3. Kuchagua biashara mbadala yenye mtaji nitakaomudu, ila wenye matapo yatakayoniwezesha kuelekea kwenye hilo lengo la pikipiki

Iwapo unahitaji msaada zaidi katika kuanzisha na kushimamisha biashara yako, usisite kuwasiliana nasi.

Managing Challenges in Persuing One´s Own Goals

The issue of academic development, starting a business or even getting a job is sometimes not easy. Especially when you are struggling to find fees, place to study, capital or business skills or even a suitable job to achieve dreams and cover living expenses, the challenges are compared to climbing a steep mountain. Sometimes there are relatives and friends comforting or supporting in one way or another. Sometimes you also have to start at a minimum and use the resources you have to implement your goals, even if the situation is unsatisfactory. In all the effort of managing these challenges, we encourage you to move forward.  If you see yourself on a crossroads and need help in managing your challenges, feel free to contact us. Over the next three months we don’t charge any costs, because your success is our priority. Again, our service does not end with advice, but we give you guidance and we will work with you until you achieve your goals.

Umuhimu wa Bima katika Kudhibiti Bajeti

Nani asiyeufahamu ule mzigo unaotokana na gharama za kuuguza mgonjwa katika familia au ule wa kufidia pengo, pale ambapo mwanafamilia anapokuwa amepoteza kazi au kipato?  Dharua kama hizi zinapotokea hazikwamishi tu mipango ya maendeleo bali huweza hata kuyumbisha uchumi binafsi na wa familia. Lile pengo ambalo zamani lilikuwa likizibwa na wanafamilia au ukoo katika dharura za ugonjwa, kifo, ukosefu wa kipato/mazao, au hata mahitaji mengine ya msingi sasa linaongezeka. Familia nyingi hufikia kikomo katika kujaribu kuhakikisha wanafamilia na wanaukoo wanapata huduma za msingi wanazozihitaji. Ukosefu wa matibabu au wa ada ya kusoma kwa baadhi ya watu, kuwepo kwa watoto wa mitaani/yatima au omba omba waliokosa msaada ni mifano michache inayothibitisha haya.

Mifuko ya hifadhi ya jamii husaidia kupunguza makali haya. Kwa kuchangia kiasi kidogo cha pesa, bima hizi hukusadia kuhifadhi kiwango chako cha maisha pale unaposhindwa kujihakikishia kipato ajili yako na familia yako kutokana na ugonjwa, ujauzito/uzazi, ulemavu, uzee, au kifo. Hata hivyo, mfuko huu unasaidia kutoa msaada nafuu na endelevu kwa ndugu yako kwa kumpilia gharama za uanachama, kwa sababu atanufaika pale atakapohitaji huduma ya afya.

Katika jedwali lifuatalo nimebainisha mifuko minne ya hitadhi ya jamii na huduma zake ili kukupatia taarifa za msingi zitakazoweza kukusaidia kufanya maamuzi sahihi katika kupangilia mambo yako. Hii orodha inahusisha Bima zinazopatikana nchi nzima ya Tanzania. Iwapo unahitaji taarifa zaidi kuhusiana na huduma zinazotolewa, tafadhali wasiliana na bima husika. Kama una swali kuhusiana na jedwali hili au una maoni, mapendekezo au hata nyongeza, karibu tuwasiliane. Kwa ushauri zaidi, wasiliana nasi pia.

No.Jina la BimaWalengwaHudumaGharama
1CHF (Common Health Insurance)
Bima ya Afya
WoteMatibabu yafuatayo katika vituo vyote vya serikali nchini Tanzania bara:
Ushauri wa daktari, vipimo vya maabara, vipimo vya picha (X-ray na ultra sound), dawa, kulazwa, upasuaji (wa Kawaida, Mdogo na Mkubwa), huduma za rufaa zilizopo ngazi ya mkoa.

Huduma zingine hazigaramikiwi
Kwa Daressalaam: Tsh. 40000/- kwa mwaka kwa mtu mmoja, Tsh. 150000/- kwa familia ya watu wasiozidi sita

Kwa mikoa mingine: Tsh. 30000/- kwa mwaka kwa familia isiyozidi watu sita
2NHIF (National Health Insurance)
Bima ya Afya
WoteHuduma ya Afya kama zilivyoorodheshwa katika tovuti ya NHIF, katika vituo vilivyosajiliwa na NHIF.
Huduma humlenga kwa mlipaji, mwenzi wake na watoto/wategemezi wanne
Bima ya Afya ya mtoto na wanafunzi wa chuo ni Tsh. 50400/- kwa Mwaka

Waajiriwa hulipia 6% ya mshahara.

Wengine wote kuanzia Tsh. 192 000/- kwa mwaka

Wastaafu katika sekta ya umma hawalipi chochote.
3NSSF (National Social Security Fund)
Bima ya Pensheni
Mwajiriwa katika sekta binafsi
Mjasiriamali katika sekta isiyo rasmi
Mafao ya kupoteza Ajira, 33.3% ya Msharaha kwa miezi 6

Mafao ya uzazi, 100% ya mshahara kwa miezi 3

Mafao ya Ulemavu

Msaada wa Mazishi, Tsh. 150 000/- mpaka 600 000/-

Mafao ya uzeeni kwanzia miaka 55 (75% ya Mshahara)

Mafao ya Urithi, malipo sawa na mafao ya uzeeni

Bima ya Afya
5% - 10% ya Mshahara kwa Mfanyakazi

Mjasiriamali hulipa kwanzia Tsh. 20 000/-
4PSSSF (Public Service Social Security Fund)

Mfuko wa hifadhi ya jamii/pensheni

Muunganiko wa mifuko ya Bima ifuatayo: PSPF (Public Services Pension Fund), LAPF (Local authorities Pension Fund), PPF (Parastatals Pensions Fund), GEPF (Government Employees Provident Fund)
Watumishi wa UmmaMafao ya kupoteza Ajria, 33.3% ya Mshahara kwa miezi 6

Mafao katika ugonjwa, 40% ya mshahara kwa miezi 3

Mkopo wa nyumba

Mafao ya uzeeni (hadi 75% ya mshahara)

Mafao ya urithi, 40% kwa mwenzi, 60% kwa watoto

Mafao ya ulemavu, malipo sawa na mafao ya uzeeni

Msaada wakati wa kifo
Mtumishi wa umma hulipia 5% ya mshahara, mwajiri 10%

Bibliogafia:

CHF. http://www.chf-iliyoboreshwa.or.tz/ (24.01.2021)

NHIF. https://www.nhif.or.tz/#gsc.tab=0   (24.01.2021)

NSSF. https://www.nssf.or.tz/ (24.01.2021)

NSSF. https://www.nssf.or.tz/index.php/news/nssf-na-psssf-warahisisha-huduma-kwa-wanachama-na-wananchi-kwa-ujumla (24.01.2021)

PSSSF.  https://www.psssf.go.tz/ (24.01.2021)

 

Happy Holidays and a Blessed New Year

Dear reader,

With few words, I would like to thank you for reading our posts, to wish you happy holidays, a happy new year and blessings in fulfilling your dreams and plans.

If this is your first visit to this page, please take a moment to review the posts listed below. We will be glad to receive your feedback.

These  posts are aimed at encouraging young people in their quest for academic and economic development, and informing them on a number of topics, e.g. how to open a business, tips on how to develop themselves academically, manage personal income e.t.c. If there is a topic you would like us to present here that may be helpful to young people, do not hesitate to write to us. Also, don’t hesitate to let others know about this site / blog so that even they can benefit from it.

We look forward to next year, when we have enough readers, to open a forum for the topics we serve on our website. For more information on our topics, see here. This forum helps interested people to exchange ideas, get to know each other, and create a network to support each other on relevant topics (for example about special training opportunities, job opportunities etc.). If you are interested, feel free to join via this form. We will keep you informed about the developent of this plan, and after we have received enough registrations, we will open the forum.

I wish you all the best for your holidays and the new year, a wonderful break from your duties and many blessings in achieving new goals in the coming year.

Namna ya kumudu gharama zako za maisha

Nani havifahamu vipindi vya hali ngumu kiuchumi ambapo unajikuta kipato chako hakitoshi kutekeleza mipango ulionayo au hata matumizi yako ya muhimu. Hasa pale dharura zinapozitokeza, k.v. matibabu, uharibifu wa mali za msingi au kupoteza kazi/kutolipwa mshahara, ni rahisi kujikuta katika changamoto kubwa ya kukidhi mahitaji binafsi. Mtu mwenye utamaduni wa kujiwekea akiba ya kutosha hata kuweza kumudu kipindi cha miezi kadhaa cha dharura au mtu mwenye vipato mbadala kutoka katika miradi mingine anaweza kuwa katika nafasi nzuri ya kumudu dharura hizi huku akiendeleza mipango yake ya maisha na ya maendeleo. Kwa sababu si wote walio na akiba au miradi hii, lazima tutazame njia zingine za kuweza kumudu gharama za maisha ambazo zaweza kufungua njia mbadala za kujihakikishia akiba. Ili kurahisisha usomaji, nimeyafupisha mawazo yangu katika dondoo zifuatazo.

  1. Bainisha matumizi au mahitaji yako ya msingi na yasiyo ya msingi. Aina na kiwango cha matumizi hutofautiana mtu na mtu, sehemu anapoishi na shughuli za uchumi anazofanya. Kwa mfano, matumizi ya mwajiriwa anayeishi kwenye nyumba ya kukodi jijini Daressalaam na kutumia usafiri wa daladala kila siku kwenda kazini ni tofauti na mjasiriamali nje ya jiji la Mwanza, anayeishi kwenye nyumba yake yenye bustani au shamba. Lisha ya tofauti hizo, matumizi yafuatayo yanaweza kukupatia mwongozo wa kupata picha ya matumizi yako: (i) Chakula, (ii) Kodi ya Nyumba, (iii) Nishati, kama vile umeme, gesi, mkaa, (iv) Gharama za Shule/Karo, (v) Mavazi, (vi) Usafi binafsi, k.v. Sabuni na vipodozi, (vii) Vifaa vya nyumbani, (viii) Bima ya afya, (ix) Mengineyo (nauli, mawasiliano, michango, burudani n.k.).

Unaweza kufupisha au kurefusha orodha hii kulingana na mahitaji yako binafsi. Kubainisha gharama halisi ulizonazo kila mwezi hukusaidia kuyaoanisha na mapato yako ya mwezi na kuhakikisha unamudu mahitaji na majukumu yako ya msingi bila shida huku ukiendelea na mipango yako ya kimaendeleo. Iwapo una mipango ya kuwekeza mahala fulani au kujikusanyia mtaji, pesa inayobaki kutoka kwenye matumizi unaweza kuitenga kila mwezi bila kuathiri hadhi au kiwango chako cha maisha. Ni wazi kuwa, kama kipato chako hakitoshi kukidhi mahitaji ya msingi, huna budi kutathmini matumizi yako na kuyapunguza au kutafuta kazi yenye kipato kinachoendana na gharama zako za maisha.

  1. Weka Akiba kwa ajili ya dharura. Dharura haipangwi, bali hujitokeza yenyewe. Na kuna dharura zinazokulenga moja kwa moja, ambazo hauwezi kukwepa, kama vile matibabu, uharibifu wa mali au kupoteza kazi/kipato. Akiba hii, ambayo hukadiriwa kuwa sawa na kipato chako cha miezi mitatu mpaka sita, ni tofauti na pesa unayoitenga katika kuwekeza katika biashara. Hii ni kwa sababu biashara yako ikiyumba, inaweza kukulazimu uchukue pesa kutoka katika mahitaji yako ya msingi na hivyo kushindwa kumudu gharama za maisha. Njia mojawapo ya kukwepa ukali wa dharura ni kuwa na Bima ya afya. Kutegemea na aina ya kifurushi utakachochukua, bima ya afya inakuwezesha kupunguza hatari ya kuichumi inayotokana na dharura ya kuugua. Kwa kulipia bima ya afya kutokana na pesa uliyoipangalia kwenye matumizi yako kila mwezi, unapata matibabu bila ya kuathiri akiba yako. Kwa mtu mwenye familia au mwenye ndugu anayehitaji matibabu ya mara kwa mara, kulipia bima ya afya sio tu ni kuwekeza kwenye afya bali ni tendo lenye uwajibikaji mkubwa, hasa katika dharura ya matibabu au pale unaposhindwa kulipia matibabu makubwa. Kulingana na utafiti wa FInscope (2017), matumizi ya matibabu yanashika nafasi ya tatu kwa umuhimu (baada ya gharama za kuishi, yaani chakula, kodi/malazi) na dharura ya kiafya/matibabu ni sababu namba moja ya watu kokopa pesa na kuingia kwenye madeni.
  2. Kuwa jasiri kuwekeza. Kuwekeza husaidia kujiongezea uwezo wako kuichumi na hukusaidia kutimiza malengo yako nje ya mahitaji yako ya kila siku. Sio kila mtu anaweza kuwa mfanya biashara mashuhuri, hasa ukiwa umeajiriwa wakati huo huo (kumbuka: ni hatari kuacha ajira iwapo biashara yako haikupi kipato cha kutimiza mahitaji ya kila siku). Tambua kipaji chako na wekeza katika talanta yako kupitia shughuli unayoiwezea vizuri. Badala ya biashara, unaweza kuboresha au kukuza bustani/shamba lako na ukajipunguzia gharama za chakula, kupata akiba ya chakula au hata kuuza na kupata fedha kwa ajili ya mipango mingine. Wengine hufuga, wengine husuka, wengine hujenga vibanda au nyumba kwa ajili ya kupangisha. Mianya ni mingi unapopata nafasi ya kujihabarisha na kubadilishana mawazo na watu. Walisiliana nasi pia kwa mawazo zaidi.

Kuna usemi usemao: „Mtu hula kulingana na urefu wa kamba yake“. Kuna hekima katika kutathmini matumizi binafsi, kujiongezea uwezo wa kipato, bila kuhatarisha mahitaji binafsi au ya familia, na kukwepa mikopo au utegemezi. Baadhi ya watu wanamudu hili jambo bila shida, wengine hupata ugumu. Iwapo unahitaji msaada zaidi, kimawazo au ushauri, usisite kujereja kwetu kupitia mawasiliano yalioko mwishoni mwa ukurasa huu. Tutafurahi sana   kukusaidia.

Barikiwa.

 

Bibliografia

Finscope Tanzania (2017). Insights that drive Innovation. https://www.fsdt.or.tz/wp-content/uploads/2017/09/Finscope.pdf

 

Namna ya Kufanikiwa katika Biashara Unayoianzisha

Kuanzisha biashara Tanzania huambatana na changamoto kadhaa kama ukosefu wa mtaji na mkakati dhaifu wa uuzaji. Lakini badala ya kuangalia sababu zinazofanya biashara kushindwa, napenda tujikite katika makala hii kwenye mambo yanayoweza kufanikisha biashara inayoanzishwa. Mawazo haya nimeyagawanya katika dondoo zifuatazo.

Tazama biashara za maeneo jirani unayoishi au biashara za watu unaowafahamu. Je, ni mambo gani yaliyofanya biashara hizo kufanikiwa, kubaki vilevile kwa muda mrefu, au hata kushindwa? Ni sababu zipi zimeleteleza matokeo hayo?

Kwa hakika kuna sababu nyingi,  zikiwemo sababu binafsi ambazo ziko nje ya uewelewa wetu. Kwa msingi huo hatuwezi tukadai kujua sababu za kila biashara kushindwa. Hata hivyo, napenda tutazame baadhi ya mambo muhimu yanayopelekea biashara kufanikiwa au hata kushindwa.

  1. Mkakati dhabiti wa uuzaji. Watanzania wanafahamu kutumia fursa katika kufanya biashara zao. Hii huusisha kufungua biashara katika maeneo yalio na watu wengi, au karibu ya kaya zao ambapo wanaweza kuduhumia kaya za jirani kwa bidhaa na huduma huku wakitimiza majukumu yao ya nyumbani. Popote pale biashara yako ilipo, ili ikue na ifanikiwe, inapaswa kujikita katika kutimiza hitaji flani la watu walioko katika eneo hilo.  Hivyo shauku ya kuanzisha biashara na kujishughulisha haina budi kuambatana na mahitaji ya msingi ya watu katika eneo husika. Ili kuweza kujua mahitaji ya wateja wako wa baadaye na kufanya uamuzi mzuri wa aina ya biashara ya kuendesha, unapaswa kufanya utafiti wa soko.
  2. Naamini unafahamu tabia ya baadhi ya watu kuelekea katika fursa flani ya biashara na kubadili mwelekeo, yaani biashara, pale wanapoona fursa nyingine. Ni kweli kuwa kupata uzoefu katika biashara tofauti tofauti huleta manufaa. Hata hivyo, swala la kubadili badili biashara lapaswa kutathminiwa kwa kina, hasa pale ambapo matokeo yake yanaathiri kipato cha familia. Kwa hakika jambo hili tunalitazama kwa utofauti, iwapo mtu ana kipato thabiti kutokana na ajira, chenye kukidhi mahitaji yake na familia yake huku “akijijaribu” katika biashara flani. Kutimiza wajibu wa riziki yako na familia yako ni muhimu huku ukijikita katika biashara yako kwa uvumilivu na kutafuta mafanikio katika biashara hiyo.
  3. Udhibiti mzuri wa mtaji. Nimekutana na baadhi ya wanafanyabiashara wanaotumia pesa au bidhaa za biashara kwa ajili ya matumizi yao binafsi (k.v. kwa ajili chakula, nauli au dharura). Hili jambo, hata kama wakati flani halikwepeki, linahitaji nidhamu kubwa. Ikarimu unaweza kuhatarisha biashara yako. Kutenganisha matumizi ya biashara na matumizi binafsi ni jambo la msingi sana. Ni kweli kuwa upatikanaji wa mtaji ni muhimu katika kuanzisha biashara. Mtu achukuaye mkopo kwa ajili ya mtaji anapaswa kutuambua deni analodaiwa na umuhimu wa kulipa deni hilo, ukizingatia kuwa kipindi cha awali cha biashara huwa kinaambatana na hasara. Kiasi kikubwa cha mkopo humaanisha pia kiasi kikubwa cha deni na kiasi kikubwa cha deni huweza kupelekea kushindwa kulipa kama pesa haidhibitiwi vizuri au ikijitokeza hasara kubwa kutoka na mauzo au wizi. Kama unakusudia kuanzisha biashara ndogo, fikiria kuhusu biashara zisizohitaji mtaji au zinazohitaji mtaji mmdogo. Kumbuka methali inayosema: “Mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe” . Jipatie mawazo kupitia mtandao au marafiki kuhusu aina za biashara zisizohitaji mkopo au zinazohitaji mkopo mdogo. Unaweza kuwasiliana nasi kwa mawazo zaidi.
  4. Jifunze kuboresha biashara yako. Kimsingi, ni vema kupata maarifa ya biashara hata kabla ya kuanza biashara. Unaweza kuona wepesi wa kufanya biashara, lakini kuwa mnyenyekevu ili kujifunza zaidi na kuepuka makosa ya kibiashara, kunaweza kukusogeza mbele zaidi. Kama umeshaanza biashara yako, jipatie muda, utoke katika mihangaiko ya biashara yako, ili ujifunze namna ya kuiboresha. Kutana na wanafanyabiashara wengine wazoefu zaidi na waliofanikiwa, pata ushauri kutoka benki, jiunge katika jukwaa la majidala au tafuta mshauri wa kitaalam ili ujifunze kutokana na uzoefu wa wengine na changamoto zao. Unaweza kufaidika sana.

Je, kuna mambo mengine ya kuzingatia katika kuendesha biashara? Tafadhali tushirikishe. Kama una swali au haja yoyote, jiskie huru kuwasiliana nasi. Kama inahitaji kufahamu zaidi kuhusu uendeshaji wa biashara, jipatie nyenzo hapa.

Nakutakia kila la kheri katika biashara yako