Kumudu Changamoto katika Kujiendeleza

Swala la kujiendeleza kimasomo, kuanzisha biashara au hata kutapata kazi wakati mwingine sio jepesi. Hasa pale unapohangaika kutafuta ada, nafasi ya chuo, mtaji au ujuzi wa biashara au hata kazi inayofaa ili kutimiza ndoto na kulisha familia, changamoto hulinganishwa na kupanda mlima mkali. Ni kweli, wakati mwingine wapo ndugu na jamaa kufariji au kuwezesha kwa namna moja au nyingine. Wakati mwingine pia unalazimika kuanza kwa kiwango cha chini na kutumia rasilimali ulizonazo ili kujiendeleza, hata kama hali hairidhishi. Katika juduhi zote za kumudu changamoto hizi,  tunakutia moyo usonge mbele. Iwapo unajiona uko katika njiapanda na unahitaji msaada katika kumudu changamoto zako, jisikie huru kuwasiliana nasi. Katika kipindi cha miezi mitatu ijayo hatuzatoza gharama yoyote, maana mafanikio yako ni kipaumbele chetu. Tena, huduma yetu haishii kwenye ushauri tu, bali tunakupatia mwongozo na tutashirikiana nawe mpaka utakapofanikisha malengo yako.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *