Timiza Ndoto Zako kupitia Biashara

Kuanzisha na kuendesha biashara inayopendwa na yenye mafanikio ni shauku ya vijana wengi. Changamoto katika kuanzisha, kuendesha na hata kuimarisha biashara tunazifahamu. Swala la kuendesha biashara limekuwa schangamoto kwa wengi kiasi kwamba wengi wanaofanikiwa kuendesha biashara, wameshindwa kujikimu kimaisha kutokana na mapato duni ya biashara zao. Takwimu zilizotolewa na Shamchiyeva, Kizu na Kahyarara kupitia shirikia la kazi duniani (ILO) linaonesha wastani wa mapato ya vijana wa kiume ni Tsh. 117,000/= kwa mwezi na kwa vijana wa kike ni 90,000/=. Japokuwa hizi takwimu zina miaka karibia kumi sasa, hata kama wastani umepanda kwa sasa ukilinganisha ni kipindi cha utafiti, haitoshi kujikimu kimaisha. Ukipiga hesabu ya pesa mtu anayohitaji kijikumu kimaisha kwa (ikihusisha chakula, kodi, usafiri, mawasiliano, afya na huduma tofauti tofauti – hata kama zinatofautianana maeneo na maeneo) lazima kiwango kisipungue laki tatu.

Wakati vijana wengi wakitafuta uhuru wa kiuchumi, kujitegemea na kuongeza kipato kupitia biashara, asilimia yao kubwa huingia kwenye biashara kwa sababu ya kukosa ajira. Changamoto hii huambatana na vijana wengi kutopangilia biashara yao vizuri – kuanzia kulenga wateja, mipango ya biashara ya muda mfupi na mrefu, na utekelezaji wa biashara hizo, kama Isai Mathias anavyoweka wazi katika waraka wake kuhusu sababu ya biashara  nyingi kufeli. Changamoto zinigine kama ukosefu wa mtaji, elimu, na uzoefu, mikopo yenye riba kubwa, upanuaji wa biashara kwa pupa, matumizi ya pesa ya biashara kwa ajili ya mahitaji binafsi, eneo baya ya biashara, na uendeshaji duni tunayafahamu.

Wakati huo huo tunafahamu kuwa uanzishaji und uendeshaji wa bia biashara – hasa kwa Tanzania ambapo mazingira huruhusu na sheria hazibani, ni fursa kubwa ya kufanya mambo na kutimiza ndoto binafsi.

Tunatambua kuwa sio kila mtu anaweza kuendesha biashara. Sio kila mtu atakuza biashara. Unaweza kutathmini uzuji/uwezo ulionao, sifa binafsi (k.v. motisha, hali ya uchumi), athari zinazoweza kujitokeza, na hali halisi, na kuchagua biashara inayokidhi mahitaji ya watu unaowalenga. Sifa hizi unaweza kujipatia. Kama unahitaji mwongozo zaidi katika kuanzisha biashara yenye mafanikio na inayoendana na mazingira uliyonayo, usisite kuwasiliana nasi. Kama unahitaji kuhudhuria mafunzo na kujijengea sifa kwa ajili ya biashara bora, usisite pia kuwasiliana nasi.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *