Umuhimu wa Bima katika Kudhibiti Bajeti

Nani asiyeufahamu ule mzigo unaotokana na gharama za kuuguza mgonjwa katika familia au ule wa kufidia pengo, pale ambapo mwanafamilia anapokuwa amepoteza kazi au kipato?  Dharua kama hizi zinapotokea hazikwamishi tu mipango ya maendeleo bali huweza hata kuyumbisha uchumi binafsi na wa familia. Lile pengo ambalo zamani lilikuwa likizibwa na wanafamilia au ukoo katika dharura za ugonjwa, kifo, ukosefu wa kipato/mazao, au hata mahitaji mengine ya msingi sasa linaongezeka. Familia nyingi hufikia kikomo katika kujaribu kuhakikisha wanafamilia na wanaukoo wanapata huduma za msingi wanazozihitaji. Ukosefu wa matibabu au wa ada ya kusoma kwa baadhi ya watu, kuwepo kwa watoto wa mitaani/yatima au omba omba waliokosa msaada ni mifano michache inayothibitisha haya.

Mifuko ya hifadhi ya jamii husaidia kupunguza makali haya. Kwa kuchangia kiasi kidogo cha pesa, bima hizi hukusadia kuhifadhi kiwango chako cha maisha pale unaposhindwa kujihakikishia kipato ajili yako na familia yako kutokana na ugonjwa, ujauzito/uzazi, ulemavu, uzee, au kifo. Hata hivyo, mfuko huu unasaidia kutoa msaada nafuu na endelevu kwa ndugu yako kwa kumpilia gharama za uanachama, kwa sababu atanufaika pale atakapohitaji huduma ya afya.

Katika jedwali lifuatalo nimebainisha mifuko minne ya hitadhi ya jamii na huduma zake ili kukupatia taarifa za msingi zitakazoweza kukusaidia kufanya maamuzi sahihi katika kupangilia mambo yako. Hii orodha inahusisha Bima zinazopatikana nchi nzima ya Tanzania. Iwapo unahitaji taarifa zaidi kuhusiana na huduma zinazotolewa, tafadhali wasiliana na bima husika. Kama una swali kuhusiana na jedwali hili au una maoni, mapendekezo au hata nyongeza, karibu tuwasiliane. Kwa ushauri zaidi, wasiliana nasi pia.

No.Jina la BimaWalengwaHudumaGharama
1CHF (Common Health Insurance)
Bima ya Afya
WoteMatibabu yafuatayo katika vituo vyote vya serikali nchini Tanzania bara:
Ushauri wa daktari, vipimo vya maabara, vipimo vya picha (X-ray na ultra sound), dawa, kulazwa, upasuaji (wa Kawaida, Mdogo na Mkubwa), huduma za rufaa zilizopo ngazi ya mkoa.

Huduma zingine hazigaramikiwi
Kwa Daressalaam: Tsh. 40000/- kwa mwaka kwa mtu mmoja, Tsh. 150000/- kwa familia ya watu wasiozidi sita

Kwa mikoa mingine: Tsh. 30000/- kwa mwaka kwa familia isiyozidi watu sita
2NHIF (National Health Insurance)
Bima ya Afya
WoteHuduma ya Afya kama zilivyoorodheshwa katika tovuti ya NHIF, katika vituo vilivyosajiliwa na NHIF.
Huduma humlenga kwa mlipaji, mwenzi wake na watoto/wategemezi wanne
Bima ya Afya ya mtoto na wanafunzi wa chuo ni Tsh. 50400/- kwa Mwaka

Waajiriwa hulipia 6% ya mshahara.

Wengine wote kuanzia Tsh. 192 000/- kwa mwaka

Wastaafu katika sekta ya umma hawalipi chochote.
3NSSF (National Social Security Fund)
Bima ya Pensheni
Mwajiriwa katika sekta binafsi
Mjasiriamali katika sekta isiyo rasmi
Mafao ya kupoteza Ajira, 33.3% ya Msharaha kwa miezi 6

Mafao ya uzazi, 100% ya mshahara kwa miezi 3

Mafao ya Ulemavu

Msaada wa Mazishi, Tsh. 150 000/- mpaka 600 000/-

Mafao ya uzeeni kwanzia miaka 55 (75% ya Mshahara)

Mafao ya Urithi, malipo sawa na mafao ya uzeeni

Bima ya Afya
5% - 10% ya Mshahara kwa Mfanyakazi

Mjasiriamali hulipa kwanzia Tsh. 20 000/-
4PSSSF (Public Service Social Security Fund)

Mfuko wa hifadhi ya jamii/pensheni

Muunganiko wa mifuko ya Bima ifuatayo: PSPF (Public Services Pension Fund), LAPF (Local authorities Pension Fund), PPF (Parastatals Pensions Fund), GEPF (Government Employees Provident Fund)
Watumishi wa UmmaMafao ya kupoteza Ajria, 33.3% ya Mshahara kwa miezi 6

Mafao katika ugonjwa, 40% ya mshahara kwa miezi 3

Mkopo wa nyumba

Mafao ya uzeeni (hadi 75% ya mshahara)

Mafao ya urithi, 40% kwa mwenzi, 60% kwa watoto

Mafao ya ulemavu, malipo sawa na mafao ya uzeeni

Msaada wakati wa kifo
Mtumishi wa umma hulipia 5% ya mshahara, mwajiri 10%

Bibliogafia:

CHF. http://www.chf-iliyoboreshwa.or.tz/ (24.01.2021)

NHIF. https://www.nhif.or.tz/#gsc.tab=0   (24.01.2021)

NSSF. https://www.nssf.or.tz/ (24.01.2021)

NSSF. https://www.nssf.or.tz/index.php/news/nssf-na-psssf-warahisisha-huduma-kwa-wanachama-na-wananchi-kwa-ujumla (24.01.2021)

PSSSF.  https://www.psssf.go.tz/ (24.01.2021)

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *