Umuhimu wa Kujiendeleza Kielimu

Kazi nyingi siku hizi zinahitaji elimu, iwe ni kwa mtu anayeingia soko la ajira, au anapoanza biashara, au kwa mtu anayehitaji kuboresha utendaji wake katika taaluma au kazi anayoifanya. Hata hivyo, kutokana na ushindani uliopo katika soko la kazi na mategemeo yaliyowekwa katika ubora wa utendaji kazi, haina budi kila mtu kujiendeleza kitaaluma. Mtu aliyesoma, kubobea katika taaluma yake, na kujipatia uzoefu wa kazi hata  katika kipindi cha uanafunzi katika kujitolea mahali, ana fursa kubwa ya kujitengenezea riziki kwa ajili yake na familia yake. Katika ngazi zote za elimu, Tanzania inatoa fursa ya kujiendeleza kielimu na kubobea katika fani au taaluma. Jedwali lifuatalo linaonesha baadhi masomo ya taaluma tofauti tofauti katika kiwango cha cheti na stashahada. Asilimia kubwa ya kozi hizi huweza kusomwa na mtu aliyehitimu elimu ya sekondari (kidato cha nne). Jedwali hili ni mfano tu unaoweka bayana kuwa kila mtu (katika kiwango chake cha elimu) anaweza kujiendeleza na kubobea katika taaluma anayopenda. Tofauti na kuanza moja kwa moja na elimu ya cheti au stashahada, kuna uwezekano wa bobea kwenye taaluma kupitia VETA, shahada au hata kozi fupi zinazotelea na taasisi tofauti tofauti za elimu. Kama una maswali zaidi au unahitaji ushauri kuhusiana na kujiendeleza kielimu, wasiliana nasi kupitia mawasiliano yetu yalioko upande wa chini wa ukurasa huu. Ili kuziona kozi ya cheti na stashahada, bonyeza hapa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *